Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, taarifa ya Kituo cha Usimamizi wa Hawza kuhusu kusimamishwa kwa shughuli za makao makuu na ofisi za usimamizi za Hawza katika mikoa wakati wa shughuli za kuaga na mazishi ya Kiongozi Mkuu wa Umma na Imam Shahidi, Ayatullah Sayyid Ali Husseini Khamenei (Quddisa Sirruhush-Sharif), ni kama ifuatavyo:
Kwa Jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu
«إِنَّا لِلَّهِ وَإِنَّا إِلَیْهِ رَاجِعُونَ»
Kwa kutoa salamu za rambirambi na maombolezo mbele ya Mtukufu Imam wa zama, Imam Al-Mahdi (roho zetu ziwe fidia kwake), na kwa taifa tukufu la Iran kufuatia kuuawa kishahidi kwa Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Imam Shahidi, Ayatullah Sayyid Ali Husseini Khamenei (Mwenyezi Mungu aitukuze na kuiinua daraja yake), na kwa kuzingatia taarifa rasmi ya Baraza Tukufu la Mawaziri kuhusu kutangaza mapumziko rasmi kwa ajili ya kufanyika kwa shughuli za kuaga, kusindikiza na mazishi ya mwili wake mtukufu, ratiba ya kusimamishwa kwa shughuli za makao makuu na ofisi za usimamizi za Hawza inatangazwa kama ifuatavyo:
1. Usimamizi wa Hawza katika Mkoa wa Tehran:
Kwa lengo la kuwezesha ushiriki wa kiwango cha juu wa wafanyakazi na watumishi wa utawala katika shughuli za mazishi, pamoja na ulazima wa kuhamasisha uwezo wote wa makao makuu ili kutoa huduma bora kwa waombolezaji, idara zote za Usimamizi wa Hawza ya Kielimu ya Mkoa wa Tehran zitafungwa kuanzia siku ya Jumamosi tarehe 13 Tir (4 July) hadi mwisho wa siku ya Jumanne tarehe 16 Tir 1405 (7 July 2026).
2. Usimamizi wa Hawza katika Makao Makuu ya Mikoa:
Ili kuwezesha mazingira yanayofaa kwa wafanyakazi na watumishi wa utawala kushiriki katika shughuli za kusindikiza mwili mtukufu katika miji ya Tehran na Qom, ofisi zote za usimamizi zilizopo katika makao makuu ya mikoa zitafungwa kuanzia siku ya Jumatatu tarehe 15 Tir (6 July) hadi mwisho wa siku ya Jumatano tarehe 17 Tir 1405 (8 July 2026).
3. Makao Makuu ya Kituo cha Hawza (Mji Mtukufu wa Qom):4
Kwa kuzingatia nafasi ya kipekee ya mji mtukufu wa Qom na uwepo wa umati mkubwa wa waombolezaji, Makao Makuu ya Kituo cha Usimamizi wa Hawza za Kielimu mjini Qom, kwa madhumuni ya kutoa huduma na msaada kwa wageni wote, mahujaji na waombolezaji wa ndani na wa kimataifa wanaohudhuria mji wa Qom kushiriki katika hafla hii kubwa ya mazishi, yatafungwa kuanzia siku ya Jumatatu tarehe 15 Tir hadi mwisho wa siku ya Jumatano tarehe 17 Tir 1405.
Kituo cha Usimamizi wa Hawza.
Maoni yako